logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond kutambulisha msanii mpya wa WCB mwezi huu wa Novemba, atangaza tarehe!

“Nov 16th / 17th 2023, tunamtambulisha SUPER STAR mpya," aliandika.

image
na Radio Jambo

Habari05 November 2023 - 09:14

Muhtasari


• Kupitia ukurasa wake wa X, awali ukijulikana kama Twitter, Diamond alitoa tangazo hilo kwa maneno machache akiandika pia tarehe.

Mkurugenzi mtendaji wa lebo ya WCB Wasafi, Diamond Platnumz ametangaza kumtambulisha msanii mwingine mkubwa katika lebo hiyo kabla ya mwezi huu wa Novemba kukamilika.

Kupitia ukurasa wake wa X, awali ukijulikana kama Twitter, Diamond alitoa tangazo hilo kwa maneno machache akiandika pia tarehe ambazo msanii huyo atazinduliwa rasmi katika sherehe kubwa itakayochukua siku mbili kumtambulisha.

Aliwapa matumaini makubwa mashabiki wake akiwaahidi kwamba hatakuwa msanii hivi hivi bali ni jina kubwa na mwenye talanta ya kupigiwa mfano, kwani siku zote Wasafi huwa si wa kubahatisha linapokuja suala la kusaini wasanii.

“Nov 16th / 17th 2023, tunamtambulisha SUPER STAR mpya, Msanii Mpya wa WCB WASAFI!!! Tunaanza Rasmi Siku Zilizosalia Kuanzia Kesho! #Wcb4Life #Wasafi” Diamond aliandika X.

Tangazo hili linaenda kinyume na tangazo ambalo alifanya mapema mwezi Julai alipokuwa akitoa tahadhari kwa wasanii wenzake kuhusu kuachia miziki kwa mfululizo hadi mwakani.

Akitoa tangazo hilo, Diamond alikuwa amedokeza kwamba angemtambulisha msanii mpya kwenye lebo ya Wasafi mapema Januari mwaka 2024, muda ambao angempisha msanii huyo kuchukua hatamu ya kuongoza kwenye trend baada ya yeye kufanya hivyo kuanzia Julai hadi Desemba mfululizo bila kutikiswa.

“Januari 2024 nitampisha msanii wangu mpya,” Diamond alisema.

“Haimanishi eti ndio kupuuza kanisa kufanya ngoma na rafiki zangu tokea Tanzania ama East Africa. Nazo zina umuhimu kwa waswahili wenzangu haswa msimu kama huu wa Wasafi Festival unavyokuja. Hivyo tegemeeni pia kumwagika kwa nyingi tu za kutosha,” Diamond alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved