logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ibada ya ukumbusho ya Jenerali Francis Ogolla yaahirishwa

Hafla ilikuwa ifanyike Ijumaa katika uwanja wa Ulinzi Sports Complex Lang’ata.

image
na Radio Jambo

Habari23 April 2024 - 06:04

Muhtasari


• Hafla hiyo ilikuwa imeratibiwa kufanyika Ijumaa, Aprili 26, 2024, katika uwanja wa Ulinzi Sports Complex huko Langata, imeahirishwa.

Ibada ya ukumbusho ya aliyekuwa mkuu wa Majeshi marehemu Jenerali Francis Omondi Ogolla, iliyokuwa imeratibiwa kufanyika Ijumaa, Aprili 26, 2024, katika uwanja wa Ulinzi Sports Complex huko Langata, imeahirishwa.

KDF, katika taarifa ya pamoja na familia ya marehemu Jenerali, ilisema kuwa tarehe mpya ya ibada ya kumbukumbu itatangazwa siku zijazo.

Taarifa hiyo haikueleza mara moja kwa nini hafla hiyo iliahirishwa, lakini ilitaja kuwa familia hiyo ilipata heshima kubwa kwa jinsi watu walijitokeza kwa maizishi ya Ogolla.

Ogolla alifariki kutokana na ajali ya helikopta Alhamisi wiki iliyopita. Ajali hiyo pia ilisababisha vifo vya maafisa tisa wa ngazi za juu katika jeshi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved