logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshambuliaji João Felix arejea Chelsea, mkataba wa miaka sita

Chelsea kuimarisha safu ya ushambuliaji baada ya kusuasua katika mechi ya ufunguzi

image
na

Habari20 August 2024 - 04:57

Muhtasari


•Mreno João Felix arejea klabu ya Chelsea kwa mkataba wa kudumu kwa kipindi cha miaka 6,baada ya kutarajiwa kufanya vipimo vya kiafya hii leo ili kuisaidia timu hiyo kujikwamua baadaya kusuasua kwa mda.

JOAO FELIX//FACEBOOK

Mreno João Felix ,24, kutoka klabu ya Atlético Madrid, sasa amekubali kujiunga na klabu ya Chelsea kutoka ligi kuu nchni Uingereza kwa mkataba wa miaka 6.Felix alikua akiichezea timu ya The Blues lakini kwa mkopo kutoka timu  ya Barcelona alipokuwa akichezea timu hiyo kwa mkopo, baada ya kucheka na nyavu mara kumi na kuchangia migongeo sita iliyozalisha mabao.

Felix atakua anajiunga na klabu hiyo ya Chelsea baada kukamilisha uhamisho wake ,ambapo vipimo vya afya vinatarajiwa kufanywa hii leo, ili kujiunga na kikosi hicho cha Enzo Maresca rasmi .

Felix alianza taaluma yake katika klabu ya Benfica, na amekua nguzo kubwa hasa akiichezea Ureno katika hatua za kitaifa na kuchangia kupatikana kwa mabao.

Baadhi ya mashabiki wa Chelsea wamefurahishwa na sajili la kinda huyo hasa ikikumbukwa alichangia pakubwa katika klabu hiyo wakati alikua mkopo kabla kwenda zake.Aidha Felix katika msimu wa 2022-23 ,alionekana kuwa mwiba  katika klabu hiyo ya Chelsea baada kufunga mabao 4, licha ya kipindi kifupi alipohudumia vijana hao wa The Blues.

Felix anatarajiwa kujumuishwa katika mechi ifutayo ili kuwania taji la ligi kuu Uingereza baada ya timu hiyo Chelsea kupteza mechi ya ufunguzi dhidi ya Man City.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved