logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Gen Z Ndio Kusema, Ole Wako Kama Utawapuuza!” Kalonzo Amwambia Ruto

Alimlaumu Ruto kwa kutotilia maanani sauti na maoni ya Gen Z kupelekea vijana hao kuanzisha kampeni dhidi ya Odinga kwenye kinyang’anyiro cha AUC ambapo walishinda baada ya Odinga kufeli.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari22 February 2025 - 13:27

Muhtasari


  • Akizungumza Ijumaa Februari 21, Kalonzo alisema kwamba mustakabli wa taifa la Kenya uko mikononi mwa Gen Z akisema kwamba vijana hao ndio wataamua uchaguzi mkuu wa 2027 

Kalonzo amuonya Ruto dhidi ya kupuuza Gen Z

KINARA wa chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka amemuonya rais William Ruto dhidi ya kuwapuuza vijana wa kizazi cha Gen Z.

Akizungumza Ijumaa Februari 21, Kalonzo alisema kwamba mustakabli wa taifa la Kenya uko mikononi mwa Gen Z akisema kwamba vijana hao ndio wataamua jinsi uchaguzi mkuu wa 2027 utakavyokuwa.

Alimtaka rais Ruto kutowapuuzilia mbali Gen Z kama watu wa kufoka kwenye mitandao ya kijamii, akisema kwamba sauti za ni za maana katika kuathiri matokeo na matukio mbalimbali nchini.

Kinara huyo mwenza wa Azimio alitolea mfano jinsi matokeo ya AUC yalivyofanyika kupelekea Raila Odinga kushindwa, akisema kwamba ni kutokana na pingamizi kali ambazo zilikumba ugombeaji wa Odinga kutoka kwa Gen Z mtandaoni.

Alimlaumu Ruto kwa kutotilia maanani sauti na maoni ya Gen Z kupelekea vijana hao kuanzisha kampeni dhidi ya Odinga kwenye kinyang’anyiro cha AUC ambapo walishinda baada ya Odinga kufeli.

“Ninaweka lawama kwa Rais William Ruto, ambaye ndiye aliyekuwa mpiga kampeni mkuu. Alikuwa na nia tofauti kwamba labda akimskuma Raila atakuwa na wakati rahisi zaidi, lakini hakujua itakuwa vigumu sana. Na pia ikumbukwe vijana wa Gen Z wako na uwezo wa kuloby, and they lobbied directly. Hii ndiyo sababu nyingine kuu ya Raila kushindwa,” Kalonzo alisisitiza.

Alisisitiza kuwa bendera ya Kenya iliyobebwa na Raila katika kampeni yake inaashiria utawala ule ule ambao ulishutumiwa kuwaua waandamanaji wasio na silaha, haswa waandamanaji wa Gen Z ambao walikabiliwa na nguvu za kikatili na vyombo vya usalama.

Ghasia zinazoshukiwa kufadhiliwa na serikali dhidi ya wanaharakati vijana, alisema, zilipunguza kwa kiasi kikubwa uungwaji mkono wa kuwania kwa Raila, kwani nchi nyingi zilihusisha mbio zake na utawala unaotawala.

“Wewe, Raila hakuwa Raila; alikuwa mgombea wa Jamhuri ya Kenya. Sasa watu wanaangalia ile bendera ya Kenya Raila alikuwa nayo pale ni the same bendera watoto walikuwa wanabeba na chupa ya maji na kufanya valid demonstrations na kuuawa, with no valid explanation. Kwa hivyo wakasema ni yule rais aliua watoto ndiye amewakilisha mgombeaji hapa,” Kalonzo alisema.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved