logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Huenda Thika Ikawa Jiji La 6 Baada Ya Ripoti Kuwasilishwa Bungeni Kiambu

HUENDA mji wa Thika ukawa jiji la 6 nchini Kenya baada ya Nairobi, Mombasa, Kisumu, Nakuru na Eldoret baada ya ripoti kuwasilishwa na gavana katika bunge la kaunti.

image
na MOSES SAGWE

Habari23 February 2025 - 08:27

Muhtasari


  • Ikikabidhiwa, litakuwa jiji la sita nchini na la kwanza katika eneo la Kati mwa Kenya.
  • Ripoti na hati hiyo ilitayarishwa na kamati ya muda iliyokuwa ikiongozwa na aliyekuwa Seneta Sylvia Kasanga, ikiangazia utayari wa mji huo kuwa jiji.

Mji wa Thika

HUENDA mji wa Thika ambao ni makao makuu ya kaunti ya Kiambu ukawa jiji la 6 nchini Kenya baada ya Nairobi, Mombasa, Kisumu, Nakuru na Eldoret baada ya ripoti kuwasilishwa na gavana katika bunge la kaunti.

Azma hiyo inayolenga kupandishwa hadhi kwa Thika kutoka mji hadi jiji imeshika kasi na sasa wawakilishi wadi watatakiwa kujadili ripoti hiyo kabla ya kuuwasilisha mswada kwenye bunge la seneti kujadiliwa.

Ikikabidhiwa, litakuwa jiji la sita nchini na la kwanza katika eneo la Kati mwa Kenya.

Ripoti na hati hiyo ilitayarishwa na kamati ya muda iliyokuwa ikiongozwa na aliyekuwa Seneta Sylvia Kasanga, ikiangazia utayari wa mji huo kuwa jiji.

Ilikabidhiwa kwa Spika wa Bunge la Kaunti na Karani wakati wa hafla iliyoandaliwa katika Jumba la Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Mount Kenya mjini Thika jana.

Wamatangi alionyesha matumaini kuwa mji utapata kupandishwa hadhi, akiongeza kuwa mabadiliko hayo yatafungua fursa mpya za maendeleo na ukuaji wa uchumi.

Alisema mji huo una uwezo wa kuvutia uwekezaji mkubwa na kuzalisha ajira kutokana na eneo lake la kimkakati, na kuongeza kuwa hadhi ya jiji itaufanya mji huo kuvutia zaidi ya Sh6 bilioni kila mwaka kwa ajili ya kuendeleza miundombinu na kutoa ajira zaidi ya 50,000 kupitia viwanda na teknolojia.

"Tunatumai kuwa haitachukua muda mrefu kabla ya kupata jiji katika Kaunti ya Kiambu, la kwanza katika eneo la Kati. Tumeingia kwenye mchakato wa kutunga sheria, ambao utaongezeka. Thika ikishakuwa jiji, itakuwa na uwezo wa kuvutia uwekezaji, maendeleo na kubuni nafasi za kazi. Pia itapunguza shinikizo katika jiji la Nairobi,” alisema gavana Wamatangi.

Kasanga alisema ripoti hiyo ni ya kina, akisema ilianza kwa ushirikishwaji wa wananchi miongoni mwa wananchi kabla ya kuandika ripoti.

Viongozi wa eneo hilo, wakiongozwa na Naibu Spika John Njiru, ambaye pia ni MCA wa Wadi ya Hospitali, walisema hadhi ya Jiji itasababisha nafasi kubwa za kazi kwa wenyeji.

Alitoa wito kwa wakazi kuunga mkono mchakato huo, akisema wanaweza kufaidika pakubwa.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved