logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Je, ni kweli Hustler Fund ilipewa watu ambao hawajazaliwa? Wizara ya Oparanya yajibu

Wasiwasi ulijitokeza katika ripoti ya ukaguzi wa fedha ikidai baadhi ya wanufaika na Hustler Fund tarehe zao za kuzaliwa zilikuwa zilitarajiwa kuanzia Julai 2024 hadi Desemba 2073.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari07 March 2025 - 11:00

Muhtasari


  • Wasiwasi ulijitokeza katika ripoti ya ukaguzi wa fedha ikidai baadhi ya wanufaika na Hustler Fund tarehe zao za kuzaliwa zilikuwa zilitarajiwa kuanzia Julai 2024 hadi Desemba 2073.
  • Hata hivyo, PS Mang’eni alitupilia mbali madai hayo, akieleza kuwa tofauti hizo zilitokana na makosa ya uchimbaji wa takwimu badala ya upotevu halisi wa fedha.

PS Susan Mang'eni

SERIKALI kupitia Wizara ya Ushirika na MSMEs imejitokeza kujitetea dhidi ya ripoti ya mkaguzi mkuu wa fedha za serikali Nancy Gathungu kuhusu ubadhirifu wa mkopo wa Hustler Fund.


Akizungumza mbele ya Kamati ya Bunge ya Kitaifa ya Idara ya Biashara, Viwanda na Ushirika ikiongozwa na Mhe. Maryanne Keitany, katibu katika wizara hiyo inayoongzwa na waziri Wycliffe Oparanya, Susan Mang’eni alikanusha vikali ripoti hiyo.


Wakati wa mkutano huo, Mang’eni alibaki na msimamo wa serikali kwamba Hustler Fund ilikuwa imetolewa kwa watoto wadogo au wanufaika wasiostahiki, akihakikishia kamati kwamba hakuna pesa zilizopotea au kutengwa vibaya.


Pia alisisitiza uadilifu wa hazina hiyo, akikariri kuwa huduma ya mkopo inasalia kuwa salama na imedhibitiwa kikamilifu.


“Takwimu zilizotumika katika ripoti ya ukaguzi zilikuwa na makosa makubwa ya uchimbaji kwa sababu ukaguzi haukufanyika katika mazingira ya moja kwa moja. Tangu wakati huo tumesafisha rekodi, na watu wote waliochukuliwa sampuli wamethibitisha vitambulisho na nambari za simu,” PS Mang’eni alieleza.


Wasiwasi ulijitokeza katika ripoti ya ukaguzi wa mwaka wa fedha wa 2023/24, ikipendekeza kuwa baadhi ya wanufaika walirekodiwa kuwa ni watu ambao hawajazaliwa, ambapo tarehe za kuzaliwa zilitarajiwa kuanzia Julai 2024 hadi Desemba 2073.


Hata hivyo, PS Mang’eni alitupilia mbali madai hayo, akieleza kuwa tofauti hizo zilitokana na makosa ya uchimbaji wa takwimu badala ya upotevu halisi wa fedha.


“Pia niliihakikishia kamati kuwa mfumo wa Hustler Fund hauruhusu watoto wadogo kupata mikopo, na hivyo kuimarisha dhamira ya serikali ya uwazi na uwajibikaji katika kusimamia mfuko huo,” Mang’eni alisasisha kupitia jukwaa la X.


 


 


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved