Fayssal Beyrouk, mshauri wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari, anatoa maelezo kuhusu miundombinu ya Bandari ya Urafiki iliyoko Nouakchott, Mauritania, Mei 21, 2025. (Xinhua/Si Yuan)

Mapema Julai, wimbo maarufu wa Auld
Lang Syne kwa lugha ya Kichina ulisikika darasani katika Taasisi ya Confucius
jijini Nouakchott, mji mkuu wa Mauritania.
Li Mo, mwalimu kutoka China,
aliwaongoza wanafunzi kuimba kwa Kichina, akiwasilisha heshima kwa urafiki
unaovuka mipaka ya lugha na taifa.
“Kila mtu hapa anaujua wimbo huu na
maana yake,” alisema Li. “Unawakilisha kwa ukamilifu urafiki wa kudumu kati ya
China na Mauritania.”
China na Mauritania ziliweka
uhusiano wa kidiplomasia mnamo Julai 19, 1965. Katika kipindi cha miongo sita
iliyopita, “urafiki” umekuwa mada kuu ya ushirikiano wao. Miradi maarufu kama
vile Bandari ya Urafiki, Hospitali ya Urafiki, na Daraja la Urafiki kati ya
China na Mauritania lililokamilika hivi karibuni, ni alama ya kudumu ya
mahusiano haya.
Iko kwenye pwani ya Atlantiki, Bandari Huru ya Nouakchott, inayojulikana pia kama Bandari ya Urafiki, inachukuliwa kuwa “pafu la uchumi” wa Mauritania. Imejengwa na kampuni ya Kichina, bandari hiyo ilianza kazi mwaka 1986.

Kabla ya ujenzi wake, Mauritania
haikuwa na bandari asilia na ilikumbwa na uhaba mkubwa wa vifaa muhimu.
Wataalam wa Ulaya waliwahi kusema kuwa bandari ya kina kirefu haingewezekana.
Kukamilika kwake kulikuwa hatua muhimu katika harakati za nchi hiyo kujitegemea
kiuchumi.
“Bila bandari, mipango mingi ya
maendeleo ya kitaifa isingeliwezekana,” alisema Fayssal Beyrouk, mshauri wa
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari, ambaye aliwahi kusomea usimamizi wa
bandari nchini China. “Bandari ya kina kirefu ilirahisisha uingizaji wa vifaa
vya viwandani na bidhaa muhimu, na kuweka msingi wa maendeleo yetu ya
kiuchumi.”
Kwa msaada wa kuendelea kutoka
China, bandari hiyo imepanuliwa mara kadhaa. Kufikia mwaka 2024, uwezo wake wa
kushughulikia mizigo ulikuwa tani milioni 6.12 kwa mwaka, ikiwa ni pamoja na
makasha ya futi ishirini 230,000—takriban asilimia 80 ya biashara ya nje ya
nchi hiyo.
“Leo, bandari haitumiki tu kwa Mauritania bali pia inajitokeza kama kitovu cha usafirishaji kwa majirani wasio na bandari kama Mali,” alisema Ahmedou Mokhtar El Gayed, meneja wa biashara wa bandari hiyo. “Eneo maalum la kiuchumi linapangwa kuanzishwa ndani ya bandari hiyo ili kusaidia sekta ya mafuta na gesi. Hakuna hata moja kati ya haya lingekuwa linawezekana bila msaada thabiti kutoka China.”

Ahmedou Mokhtar El Gayed, meneja wa biashara wa Bandari ya Urafiki, akitazama meli bandarini huko Nouakchott, Mauritania, Juni 19, 2025. (Xinhua/Si Yuan)
Mradi mwingine mkubwa wa
miundombinu, Daraja la Urafiki kati ya China na Mauritania, ulizinduliwa Mei
mwaka huu. Daraja hilo lililojengwa na kampuni ya Kichina kando ya Barabara ya
Kitaifa N2 jijini Nouakchott, limepunguza msongamano wa magari na kuwa kivutio
maarufu kwa wakazi.
Mbali na kuboresha usafiri, mradi
huo uliunda nafasi za ajira. Katika kilele chake, wafanyakazi 320 wa Mauritania
waliajiriwa. Wahandisi wa Kichina waliwafundisha wafanyakazi wa eneo hilo stadi
muhimu za kiufundi, ikiwa ni pamoja na kazi za chuma, upimaji ardhi, na
uchunguzi wa vifaa.
“Wengi wa wafanyakazi
tuliowafundisha walikuja kuajiriwa kwenye miradi mingine—hii ni ishara ya
kuthaminiwa kwa ujuzi wao,” alisema Zhang Huijie, mkuu wa timu ya kiufundi ya
mradi huo.
Ushirikiano katika sekta ya afya pia
umezaa matokeo makubwa. Hospitali ya Urafiki iliyojengwa kwa msaada wa China
mwaka 2010 ni mojawapo ya hospitali kubwa za umma jijini Nouakchott. Iko katika
wilaya ya Arafat na inahudumia takriban asilimia 60 ya wakazi wa kipato cha chini
na cha kati wa jiji hilo.
“Marafiki wetu kutoka China wametupa
msaada mkubwa,” alisema mkurugenzi wa hospitali Mustafa Abdallahi. “Mbali na
kujenga hospitali, wanaendelea kutoa vifaa vya matibabu, dawa, na msaada wa
kiufundi.”
Tangu mwaka 1968, China imetuma timu 35 za madaktari nchini Mauritania. Zaidi ya madaktari na wataalamu 800 wa Kichina wamekuwa wakitoa huduma za muda mrefu. Timu ya sasa inaendesha kliniki ya tiba ya jadi ya Kichina (TCM) katika hospitali hiyo, ambapo matibabu ya sindano (acupuncture) kwa maumivu ya mgongo, shingo, na viungo yamekuwa maarufu zaidi.

“Watu hupanga foleni kwa ajili ya
ushauri wa TCM kila tunapofungua,” alisema Liu Sijia, mmoja wa wanachama wa
timu hiyo. “Tunawafundisha pia madaktari wa hapa ili kusaidia kusambaza maarifa
haya muhimu.”
Akizungumza na Shirika la Habari la
Xinhua, Balozi wa China nchini Mauritania Tang Zhongdong alisema kuwa
Mauritania imependekeza miradi zaidi ya maendeleo ipewe chapa ya “Urafiki” kama
ishara ya kuaminiana kwa pande zote mbili na uhusiano wa muda mrefu wa
kirafiki.
“Miradi zaidi ya ‘Urafiki’ inakuja,” alisema Tang. “Itaendelea kuinua uhusiano wa China na Mauritania kufikia viwango vipya.”