logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jukwaa la vyombo vya habari la China–DRC lakuza ushirikiano wa kunufaishana na pande zote

“Ushirikiano kati ya Afrika na China umetoa msaada muhimu kwa maendeleo ya bara la Afrika.”

image
na XINHUA

Kimataifa19 March 2026 - 13:04

Muhtasari


    Fu Hua, rais wa Shirika la Habari la Xinhua, akitoa hotuba kwa njia ya video katika hafla ya ufunguzi wa Jukwaa la Vyombo vya Habari la China na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), mjini Kinshasa, DRC, Machi 18, 2026. Jukwaa la Vyombo vya Habari la China–DRC lilifanyika Jumatano mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC. (Xinhua/Yang Guang)

    Jukwaa la Vyombo vya Habari kati ya China na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) lilifanyika Jumatano mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC.

    Likibeba kaulimbiu “Uboreshaji wa Kisasa wa China na Njia ya Maendeleo ya DRC: Kuchunguza kwa Pamoja Njia Mpya za Kunufaishana na Ushirikiano wa Pande Zote,” jukwaa hilo lilivutia takriban washiriki 250 wakiwemo wanasiasa, wawakilishi wa vyombo vya habari na viongozi wa biashara kutoka nchi hizo mbili.

    Katika hotuba ya video wakati wa ufunguzi, Rais wa Shirika la Habari la Xinhua, Fu Hua, alibainisha kuwa mwaka huu unaadhimisha miaka 70 tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na mataifa ya Afrika, pamoja na kuwa mwaka wa China–Afrika wa mabadilishano ya watu kwa watu.

    Alisema Xinhua itatumia jukwaa hilo kama fursa ya kushirikiana na vyombo vya habari vya DRC kuelezea kwa kina dira iliyowekwa na viongozi wa nchi hizo mbili.

    Xinhua inalenga kusimulia hadithi zenye mvuto kuhusu ushirikiano wa pande mbili, kuchunguza masuala ya kimkakati yanayohusu maendeleo ya China na Afrika, na kuandaa shughuli za kubadilishana uzoefu kama vile Jukwaa la Vyombo vya Habari na Taasisi za Tafiti za Global South, aliongeza.

    Hatua hizi, alisema, zitasaidia kuimarisha uwakilishi na sauti ya nchi hizo katika mfumo wa utawala wa kimataifa, pamoja na kuongeza nguvu mpya katika maendeleo endelevu ya ushirikiano kati ya China na Afrika.

    Naibu Waziri Mkuu wa DRC na Waziri wa Uchumi wa Taifa, Daniel Mukoko Samba, alisema uhusiano wa muda mrefu kati ya China na DRC umeendelea kujengwa juu ya msingi wa ushirikiano na urafiki.

    Aliongeza kuwa ushirikiano kati ya Afrika na China umechangia pakubwa maendeleo ya bara la Afrika.

    Mukoko alisisitiza kuwa vyombo vya habari vina jukumu muhimu la kuwa daraja la kuimarisha uelewano kati ya wananchi wa nchi hizo mbili na kukuza ushirikiano wao.

    Kwa upande wake, Waziri wa Mawasiliano na Vyombo vya Habari wa DRC na msemaji wa serikali, Patrick Muyaya, alisema jukwaa hilo linaashiria hatua mpya katika ushirikiano wa vyombo vya habari kati ya DRC na China.

    Alitoa wito kwa pande zote kuimarisha ushirikiano wa taasisi, kuchunguza matumizi ya teknolojia mpya kama mageuzi ya kidijitali na akili bandia katika usambazaji wa habari, kukabiliana kwa pamoja na changamoto ya habari za uongo, na kuendeleza mahusiano ya pande mbili.

    Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habari la Congo (ACP), Bienvenu Bakumanya, alisema jukwaa hilo linaonyesha kuwa ushirikiano wa vyombo vya habari kati ya nchi hizo unaingia katika hatua ya utekelezaji wa vitendo.

    Alihimiza vyombo vya habari vya nchi hizo mbili kubeba jukumu la kuwa “wabunifu wa mawasiliano” kwa kuonesha kwa kina manufaa halisi ya kijamii, kiuchumi na kiteknolojia yanayotokana na ushirikiano wao.

    Balozi wa China nchini DRC, Zhao Bin, alisema mahusiano ya sasa kati ya China na DRC yako katika hatua mpya ya kihistoria, huku maendeleo ya kisasa ya China yakitoa fursa zaidi kwa maendeleo na ustawi wa DRC.

    Akibainisha kuwa jukwaa hilo linafungua mfululizo wa shughuli za mwaka wa mabadilishano ya watu kwa watu kati ya China na Afrika nchini DRC, Zhao alieleza matumaini kuwa vyombo vya habari vya pande zote vitaendelea kuangazia mafanikio ya ushirikiano wa vitendo na kusimulia hadithi za urafiki kati ya wananchi wa nchi hizo mbili.

    Jukwaa hilo liliandaliwa kwa pamoja na Shirika la Habari la Xinhua na ACP, na pia lilijumuisha maonesho ya picha yanayoonyesha mafanikio ya ushirikiano kati ya China na DRC.

    Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Waziri wa Uchumi wa Taifa, Daniel Mukoko Samba, akihutubia hafla ya ufunguzi wa Jukwaa la Vyombo vya Habari la China–DRC mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC, Machi 18, 2026.Jukwaa la Vyombo vya Habari la China na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) lilifanyika Jumatano mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC.Likibeba kaulimbiu “Uboreshaji wa Kisasa wa China na Njia ya Maendeleo ya DRC: Kuchunguza kwa Pamoja Njia Mpya za Kunufaishana na Ushirikiano wa Pande Zote,” jukwaa hilo lilivutia takriban wanasiasa 250, wawakilishi wa vyombo vya habari na viongozi wa biashara kutoka nchi hizo mbili. (Xinhua/Yang Guang)
    Patrick Muyaya, Waziri wa Mawasiliano na Vyombo vya Habari wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na msemaji wa serikali, akihutubia hafla ya ufunguzi wa Jukwaa la Vyombo vya Habari la China–DRC mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC, Machi 18, 2026.Jukwaa la Vyombo vya Habari la China na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) lilifanyika Jumatano mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC. Likibeba kaulimbiu “Uboreshaji wa Kisasa wa China na Njia ya Maendeleo ya DRC: Kuchunguza kwa Pamoja Njia Mpya za Kunufaishana na Ushirikiano wa Pande Zote,” jukwaa hilo lilivutia takriban wanasiasa 250, wawakilishi wa vyombo vya habari na viongozi wa biashara kutoka nchi hizo mbili. (Xinhua/Yang Guang)
    Bienvenu Bakumanya, mkurugenzi mkuu wa Shirika la Habari la Congo (ACP), akihutubia hafla ya ufunguzi wa Jukwaa la Vyombo vya Habari la China na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC, Machi 18, 2026.Jukwaa la Vyombo vya Habari la China na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) lilifanyika Jumatano mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC. Likibeba kaulimbiu “Uboreshaji wa Kisasa wa China na Njia ya Maendeleo ya DRC: Kuchunguza kwa Pamoja Njia Mpya za Kunufaishana na Ushirikiano wa Pande Zote,” jukwaa hilo lilivutia takriban wanasiasa 250, wawakilishi wa vyombo vya habari na viongozi wa biashara kutoka nchi hizo mbili. (Xinhua/Yang Guang)

    Washiriki wa jukwaa wanatazama maonesho ya picha kuhusu mafanikio ya ushirikiano kati ya China na Jamhuri ya Kidemokrasiaya Congo (DRC) wakati wa Jukwaa la Vyombo vya Habari la China–DRC mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC, Machi 18, 2026. Jukwaa la Vyombo vya Habari la China na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) lilifanyika Jumatano mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC. Likibeba kaulimbiu “Uboreshaji wa Kisasa wa China na Njia ya Maendeleo ya DRC: Kuchunguza kwa Pamoja Njia Mpya za Kunufaishana na Ushirikiano wa Pande Zote,” jukwaa hilo lilivutia takriban wanasiasa 250, wawakilishi wa vyombo vya habari na viongozi wa biashara kutoka nchi hizo mbili. (Xinhua/Yang Guang)

    Washiriki wa jukwaa wanawasili katika ukumbi wa Jukwaa la Vyombo vya Habari la China na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC, Machi 18, 2026. Jukwaa la Vyombo vya Habari la China na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) lilifanyika Jumatano mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC. Likibeba kaulimbiu “Uboreshaji wa Kisasa wa China na Njia ya Maendeleo ya DRC: Kuchunguza kwa Pamoja Njia Mpya za Kunufaishana na Ushirikiano wa Pande Zote,” jukwaa hilo lilivutia takriban wanasiasa 250, wawakilishi wa vyombo vya habari na viongozi wa biashara kutoka nchi hizo mbili. (Xinhua/Yang Guang)


    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved