logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jukwaa la wafadhili wa Global South 2026 kufanyika Beijing

Jukwaa la Wafadhili wa Global South 2026 limepangwa kufanyika kuanzia Machi 25 hadi 26 mjini Beijing

image
na XINHUA

Kimataifa23 March 2026 - 12:49

Muhtasari


    Jukwaa la Wafadhili wa Global South 2026 linatarajiwa kufanyika kuanzia Machi 25 hadi 26 mjini Beijing.

    Likibeba kaulimbiu “Kuangaza Global South,” tukio la mwaka huu litaangazia mada kuu ya “kuongoza ukwasi wa kijani wa mitaji ya kimataifa.”

    Litawakutanisha viongozi wa taasisi za kifedha, wataalamu na wadau wa sekta kutoka China na mataifa mengine kujadili mifumo ya maendeleo ya kifedha inayolingana na mahitaji ya Global South, kwa lengo la kuleta msukumo mpya katika uthabiti na ustawi wa uchumi wa dunia.

    Imebainika kuwa baraza la jukwaa hilo litazinduliwa kama mfumo wa uendeshaji wa muda mrefu, likianzisha utaratibu wa mara kwa mara wa kupanga ajenda, kuratibu rasilimali na kuwezesha ushirikiano mwaka mzima.

    Wakati huo huo, faharasa inayolenga maendeleo ya biashara ya kijani katika nchi za Global South itazinduliwa katika jukwaa hilo. Kituo cha maonesho ya suluhisho za uendelevu pia kitafunguliwa, huku Mkutano wa Tatu wa Ushirikiano wa Taarifa za Kiuchumi wa Ukanda na Njia (BREIP) ukitangazwa.

    Kupitia hotuba kuu, mihadhara ya wataalamu na mijadala ya mezani, wawakilishi kutoka mashirika ya kimataifa, vyombo vya udhibiti wa kifedha, taasisi za kifedha, taasisi za utafiti, vyuo vikuu na makampuni makubwa watajadili masuala muhimu kama vile “ukwasi wa mtaji wa kijani.”

    Aidha, jarida la kimataifa kuhusu fedha za Global South litazinduliwa katika jukwaa hilo, likilenga kuimarisha sauti ya Global South katika masuala ya kifedha ya kimataifa.

    Jukwaa hilo litaandaliwa na Ofisi ya Kazi za Chapa ya Shirika la Habari la Xinhua, China Economic Information Service (CEIS), Kituo cha Taifa cha Taarifa za Kifedha, China Securities Journal, Shanghai Securities News, Economic Information Daily, na China Fortune Media Group. Fenjiu Group ni mshirika mkuu, huku Benki ya Kilimo ya China (ABC) ikiwa mshirika wa kimkakati. Kampuni ya Zeekr itatoa huduma za magari kwa jukwaa hilo.

    Skana msimbo wa QR kisha uubebe/kutuma kwenye simu yako ya mkononi.


    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved