logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tujiteme sana, umaskini unadhalilisha - Irene Uwoya

Irene Uwoya awataka mashabiki wake kujituma katika maisha ili kuepuka dharau inayoletwa na umaskini.

image
na

Makala20 April 2022 - 12:24

Muhtasari


• Irene Uwoya amewataka mashabiki wake kujituma kwa kile alikitaja kuwa umaskini unapotezea mtu heshima katika jamii.

• Kulingana naye unapokuwa na hela kuna mambo mengi ambayo unawezakuyafanya.

Mwanafilamu na mfanyibiashara kutoka Tanzania, Irene Uwoya amewataka mashabiki wake kupambana zaidi katika maisha kwani umaskini unadhalilisha.

Kupitia ujumbe ambao alichapisha katika ukurasa wake wa Instagram, Uwoya alisema kwamba umaskini unamfanya mtu kukosa umuhimu na kudharauliwa katika jamii.

"Tupigane sana umaskini unadhalilisha sana," Uwoya aliandika.

Uwoya anafahamika kwa hulka yake ya kuishi maisha ya juu, ikionyesha kwamba anajituma kuhakikisha anadumisha kiwango hicho cha maisha.

Mashabiki nao walionekana kukubaliana naye kwa jinsi ambavyo amewamotisha kina dada wengi, kutokana na mitindo yake ya kimaisha.

"Nakuelewa na miondoko yako sana, swaga zako ni za kibabe," shabiki mmoja aliandika.

Wengine walisema kwamba ukiwa maskini hata wandani na wanafamilia hukosa kukuheshimu kwa kuwa huna la mno unalochangia.

Je wewe unakubaliana kwamba ukosefu wa hela unasababisha dharau katika jamii?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved