logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makamishna wawili na Mkurugenzi Mtendaji wa IEBC wamejeruhiwa- Chebukati

Chebukati alibainisha kuwa baadhi ya wafanyakazi wake pia wameathirika.

image
na Radio Jambo

Habari15 August 2022 - 15:12

Muhtasari


•Mweneyikiti wa IEBC Wafula Chebukati alibainisha kuwa baadhi ya wafanyakazi wake pia wameathirika.

akizungumza katika Bomas of Kenya mnamo Agosti 10, 2022

Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati sasa anasema wawili wa kamishna wake na Mkurugenzi Mtendaji wa IEBC wamejeruhiwa na kwa sasa wanapokea matibabu hospitalini.

Akizungumza siku ya Jumatatu kabla ya kutangaza matokeo ya urais, Chebukati alibainisha kuwa baadhi ya wafanyakazi wake pia wameathirika.

Alidai kuwa baadhi walikamatwa kutoka kituo cha kitaifa cha kujumuisha kura kilichopo Bomas na hakuna sababu zilizotolewa kwa ajili hiyo.

"Haikuwa safari rahisi, hivi sasa makamishna wangu wawili na Mkurugenzi Mtendaji wamejeruhiwa na wanatibiwa. Wafanyikazi wetu wametambulishwa. Msimamizi wa uchaguzi eneo la Embakasi Mashariki alitoweka akiwa kazini," Chebukati alisema.

Alisema ametishwa, lakini ana jukumu la kuwatumbuiza Wakenya.

“Tuna watumishi ambao wamekamatwa ovyo bila sababu, wengine wanaunda kituo hiki lakini tuna wajibu wa kikatiba kufanya kazi ndiyo maana nasimama mbele yenu licha ya vitisho.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved