logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nani ataongoza IEBC? Majina 37 ya waliiomba nafasi ya mwenyekiti yafichuliwa

Tume ya uteuzi wa IEBC ina jukumu la kuwachagua mwenyekiti mpya na makamishna sita ndani ya siku 90.

image
na Samuel Mainajournalist

Yanayojiri06 March 2025 - 13:16

Muhtasari


  • Aliyekuwa Msajili Mkuu wa Idara ya Mahakama Anne Amadi na Jaji wa zamani wa Mahakama ya  EACJ Charles Nyachae, wamewasilisha maombi.
  • "Baada ya bunge kukamilisha mchakato wa kuhakiki wagombea, tume mpya itaapishwa na kuchukua majukumu rasmi," alisema Kiome.

IEBC

Jumla ya watu 37, akiwemo aliyekuwa Msajili Mkuu wa Idara ya Mahakama Anne Amadi na Jaji wa zamani wa Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki (EACJ) Charles Nyachae, wamewasilisha maombi yao kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa IEBC.

Tume ya uteuzi wa IEBC, ambayo ilitangaza majina hayo Alhamisi, ina jukumu la kuwachagua mwenyekiti mpya na makamishna sita ndani ya siku 90.

Miongoni mwa wagombea nafasi wengine mashuhuri ni mwenyekiti wa bodi ya KPLC, Joy Brenda Masinde-Mdivo, aliyekuwa Afisa Mkuu Mtendaji wa IEBC James Oswago, na wakili Francis Kissinger.

Kamati hiyo inalenga kukamilisha mchakato wa uteuzi ifikapo Mei. Kulingana na Makamu Mwenyekiti wa Paneli, Lindah Kiome, majina ya waliofaulu yatawasilishwa kwa Rais mnamo Aprili 25 kabla ya kupelekwa Bungeni kwa uchunguzi.

"Baada ya bunge kukamilisha mchakato wa kuhakiki wagombea, tume mpya itaapishwa na kuchukua majukumu rasmi," alisema Kiome.

Tangazo lililochapishwa kwenye gazeti la humu nchini tarehe 6 Machi 2025 liliorodhesha wagombea wote 37. Miongoni mwao ni Abdulqadir Lorot H. Ramadhan, Cedrick Ogoro Mukhwana, Choge Rollince, Calistus Wekesa Waswa, Duncan Oburu Ojuwang, Erastus Edung Ethekon, Chrisphine Otieno Owiye, Fred Khaemba Musungu, Edward Katama Ngeywa, na Isaac Mutie Mutua.

Wengine wanaowania nafasi hiyo ni Jackson Angoturum, Jacob Nyekele Mwegei, James Humphrey Obanda Oswago, Josiah Onyancha, Justry Patrick Lumumba Nyaberi, Kadhua Jimmy Kahindi, Kenneth Kiplimo Kemboi, Kibet Victor, Lilian Wanjiku Manenge, Nelly Peris Ashubwe, na Patrick Omutia Otulia.

Orodha hiyo pia inajumuisha Peterkin Nyongesa, Samson Omua Ogada, Samuel Kariuki Kiragu, Samuel Osewe Ochillo, Saul Simiyu Wasilwa, Thomas Maosa Nyakambi, Vincent Omondi Olouch, Walubengo Waningilo, William Otieno Oketch, Wilson Wambugu Maina, Wycliffe Kiprotich Kiprono Bonnke, na Yvonne Mercy Olaka.

Kulingana na kamati ya uteuzi, jumla ya maombi 1,848 yaliwasilishwa kabla ya tarehe ya mwisho ya Februari 15. Baada ya kuondoa maombi yaliyofanana na yasiyokamilika, idadi hiyo ilipunguzwa hadi wagombea 37 waliotimiza vigezo vya awali.

Mwenyekiti wa paneli hiyo, Nelson Makanda, alithibitisha kuwa mchakato wa kupunguza idadi ya wagombea uko mbioni.

"Tutatangaza orodha fupi hivi karibuni kisha kuanza hatua ya mahojiano," alisema kwenye taarifa rasmi.

Mchakato wa uteuzi unafuata matakwa ya kisheria, ambapo Mwenyekiti wa IEBC anatakiwa kuwa na angalau miaka 15 ya tajriba kama jaji wa mahakama kuu au uzoefu wa kiwango cha juu kama mtaalamu wa sheria, hakimu, au msomi wa taaluma ya sheria.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved