logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tindi Mwale ambwaga Otiende Amollo kutwaa uwenyekiti wa PAC

Mwale alimbwaga mpinzani wake Mbunge wa Rarieda Otiende Amollo kwa kura tisa dhidi ya sita za Otiende.

image
na Davis Ojiambo

Yanayojiri12 March 2025 - 18:45

Muhtasari


  • Mwale amekuwa akihudumu kama kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, tangu mwenyekiti aliyekuwepo John Mbadi alipoteuliwa kuwa waziri wa fedha.
  • Pokot Kusini David Pkosing amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji wa Umma kuhusu Masuala ya Biashara na Nishati bila kupingwa.
  • Mbunge wa Turkana Kusini John Ariko akichaghuliwa naibu mwenyekiti

Mwenyekiti wa Kamati PAC  Mbunge wa Butere Tindi Mwale, baada ya uchaguzi wa kamati Machi 12, 2025

Mbunge wa Butere Tindi Mwale amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge la Kitaifa ya Uhasibu wa Umma (PAC).

Mwale alimbwaga mpinzani wake wa karibu, Mbunge wa Rarieda Otiende Amollo kwa kura tisa dhidi ya sita za Otiende.

Mwale amekuwa akihudumu kama kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, tangu mwenyekiti aliyekuwepo John Mbadi alipoteuliwa kuwa waziri wa fedha.

Mwakilishi wa Wanawake wa Garissa Amina Siyad alimshinda Mbunge wa Funyula Dkt Wilberforce Oundo kutwaa nafasi ya naibu mwenyekiti.

Wakati huo huo Mbunge wa Pokot Kusini David Pkosing amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji wa Umma kuhusu Masuala ya Biashara na Nishati bila kupingwa.

Alihifadhi kiti hicho katika huku Mbunge wa Turkana Kusini John Ariko akichaghuliwa naibu mwenyekiti.

Pkosing aliwashukuru wanachama wa kamati hiyo na viongozi wa serikali mahuluti (Broad Based government) - Rais William Ruto na Raila Odinga—kwa kumkabidhi jukumu hilo.

"Ninaamini huu ni mwanzo wa uwiano na utangamano kati ya Waturkana na Pokot," Mbunge wa Laikipia Magharibi Sarah Korere alisema.

Pkosing alisema kuteuliwa kwake na Ariko ni ushahidi kwamba jamii hizo mbili si maadui. Akisema kamati hiyo itayapa kipaumbele maswala muhimu yanayohusu wananchi.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved