logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kenya Power yatangaza kukatika kwa umeme katika kaunti 9 leo, Jumanne

Umeme utakatika kwa nyakati tofauti kati ya saa mbili asubuhi hadi saa kumi na moja jioni, kutegemea eneo.

image
na Samuel Mainajournalist

Yanayojiri08 April 2025 - 07:44

Muhtasari


  • KPLC imetangaza kukatika kwa umeme katika maeneo mbalimbali ya kaunti tisa siku ya Jumanne, Aprili 8, ili kuruhusu matengenezo.
  • Kaunti zitakazoathirika ni Nairobi, Nyandarua, Uasin Gishu, Tharaka Nithi, Nyeri, Laikipia, Siaya, Kisii na Kirinyaga.

Kenya Power technicians

Kampuni ya kusambaza umeme nchini Kenya Power (KPLC) imetangaza kukatika kwa umeme katika maeneo mbalimbali ya kaunti tisa siku ya Jumanne, Aprili 8, ili kuruhusu matengenezo ya mifumo ya usambazaji wa umeme.

Kaunti zitakazoathirika ni Nairobi, Nyandarua, Uasin Gishu, Tharaka Nithi, Nyeri, Laikipia, Siaya, Kisii na Kirinyaga.

Umeme utakatika kwa nyakati tofauti kati ya saa mbili asubuhi hadi saa kumi na moja jioni, kutegemea eneo.

Nairobi

Sehemu za Nairobi zitakumbwa na kukatika kwa umeme kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni. Maeneo yatakayoathirika ni:

  • Sehemu ya Barabara ya Karen
  • Mbagathi Ridge
  • Cemastea
  • Oloolua Nature Trail Primate Research
  • Gitamuri na maeneo ya karibu

Nyandarua

Katika kaunti ya Nyandarua, maeneo yote ya Kinamba yatakosa umeme kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni. Maeneo hayo ni:

  • Muthengera
  • Kwanjiku
  • Mochongoi
  • Kabel
  • Tandare
  • Kamwenje
  • Oljabet
  • Gatundia
  • Karaba
  • Mutanga
  • Sipli
  • Olmora

Uasin Gishu

Maeneo ya Uasin Gishu yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa tisa alasiri. Maeneo ni:

  • Kipkenyo
  • Tuiyo
  • Leemok
  • Simat
  • Kaptinga
  • St. Teresa na wateja wa karibu

Siaya

Maeneo ya Siaya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni. Maeneo husika ni:

  • Nyumbani Shop
  • Shule ya Msingi ya Anduro
  • Soko la Randago
  • Shule ya Upili ya Matera
  • Soko la Tingwangi
  • Shule ya Upili ya Nyajuok
  • Booster ya Safaricom ya Nyanginja
  • Vyuo vya Ufundi vya Nyala
  • Soko la PapGori
  • Shule ya Upili ya Ojwando na maeneo ya karibu

Kisii

Katika kaunti ya Kisii, taasisi na masoko kadhaa yatakosa umeme kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni. Maeneo hayo ni:

  • Shule ya Upili ya St. Peters Keberesi
  • Magenge Secondary
  • Soko la Riokindo
  • Riokindo Boys
  • Bouster
  • Nyangeti Secondary
  • Soko la Nyabitunwa
  • Nyabiore Secondary
  • Soko la Getenga
  • Soko la Mageche
  • Nyamesocho Secondary
  • Soko la Geteni
  • Mokomoni Secondary
  • Jerusaremu
  • Nyamodo

Nyeri

Kaunti ya Nyeri itakumbwa na kukatika kwa umeme kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni. Maeneo yatakayoathirika ni:

  • Soko la Kabiru-ini na maeneo ya karibu (Kabiru-ini Kwa Gachau, Shule ya Upili ya Kabiru-ini, na Kiwanda cha Kahawa cha Kabiru-ini)
  • Soko la Kiamariga
  • Kiamariga Secondary School
  • Kituo cha Polisi cha Kiamariga
  • Shule ya Msingi ya Kianjau
  • Kijiji cha Kianjau
  • Milima ya Nyana
  • Kijiji cha Njathe-ini
  • Githiringo TBC
  • Kijiji cha Gikiriri
  • Kiamariga Hombe
  • Booster za Safaricom na Airtel

Kirinyaga

Kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni, maeneo yafuatayo katika kaunti ya Kirinyaga yatakosa umeme:

  • Chuo Kikuu cha Kirinyaga
  • Kutus Old Town
  • Kijiji cha Gitwe
  • Soko la Karia
  • Soko la Kiamwenja
  • Shule ya Upili ya Ngaru
  • Kiwanda cha Kahawa cha Karia
  • Hosteli za Ngomongo na maeneo jirani

Tharaka Nithi

Umeme utakosekana katika kaunti ya Tharaka Nithi kuanzia saa mbili na nusu asubuhi hadi saa kumi jioni katika maeneo yafuatayo:

  • Soko la Ndagani
  • Seminari ya Fransaian
  • St. Lucy
  • High Mark
  • Tumaini
  • KwaJustin

Laikipia

Katika Laikipia, umeme utakatika kati ya saa mbili na nusu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni katika maeneo haya:

  • Soko lote la Doldol
  • Olkinyei
  • Kiwanja Ndege
  • Illipollei
  • Kaimanjo
  • Ol-Donyiro na wateja wa karibu

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved