logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Je wajua kimo chako? Hizi ndizo athari na manufaa ya kuwa mfupi

Je wajua kimo chako? Hizi ndizo athari na manufaa ya kuwa mfupi

image
na

Dakia-udaku02 October 2020 - 03:35
ufupi

Kwa wanaume, baadhi hutamani kuwana urefu lakini Allan Mott, ambaye ni mfupi kwa 18cm kuliko wanaume wenye kimo cha wastani Canada amejikubali kwa ufupi alio nao.

Ushawahi kupendwa na watu wa jinsia ya pili popote unapokwenda?

Ndio yalionikuta nikiwa shuleni. Nilipotokeza tu, wasichana wakubwa walikuwa wakipiga kelele kwa furaha na kunifukuza mpaka nashindwa kuimbia tena. Wanaponikamata, wananikumbatia na kunibusu shavuni kabla ya kuniachilia niende nikacheze au nifukuzwe tena na mwingine.

Kuanzia kukabiliwa na mapenzi hayo mpaka kuishia kuwa tu mvulana mdogo darasani. Nilikuwa mcheshi , lakini kutokana na kuanza kuchezewa shere , niliondoka mara nyingi na kwenda kwenye maktaba kusaidia kupanga vitabu wakati watoto wenzangu wakicheza.

Wakati nikikuwa, daktari wa watoto alikadiria kwamba pengine huenda nikarefuka hadi 167cm, au pengine hata 172cm nikibahatika, ambacho ndicho kimo kinachokaribiana na wasatani wa urefu wa mwanamume nchini Canada.

Lakini makadirio hayo yalikuwa mbali mno na uhalisi. Niliacha kurefuka baada ya kuadhimisha miaka 13 tangu kuzaliwa. Niliishia kuwa na urefu wa 157cm, ambazo ni 10cm juu yakimo cha mbilikimo.

katika miaka iliyopita tangu hapo. Nimeishia kuamini mambo mawili kuhusu kuwa mtu mfupi .

1. Sio jambo zuri

2. Hakuna anayetaka kukusikia ukilalamika kulihusu

Huwa sipendi kulizungumzia. watu wameshaahi kuniambia, "Hebu tueleze, yaani watu hawajawahi kukuchukulia tofuati kwasababu wewe ni mfupi!" (Kila anayenimabia hili kwa kawaida ana urefu wa angalau 180cm.)

Lakini najua uhalisi wa maana ya kuwa mtu mfupi katika jamii yetu. Kuna unyanyasaji mkubwa kuhusu urefu kama ilivyokuwa kuhusu masuala ya jinsia, kabila na hata dini.

Sio siri kwamba wanawake hulipwa pesa kidogo kuliko wanaume kwa kazi sawa. Kitu ambacho watua wanastahili kujua ni kwamba urefu wa mtu ni suala muhimu katika utofauti wa mishahara.

wanaume wafupi hufunzwana jamii kujikubali na kukubali chochote wanachopata. Ninapopata kazi na niependekezewa mshahara kiwango fulani, hisia ninayokuwa nayo ni: "Ni chini ya kiwango nilichotarajia, ahh lakini sawa nitachukua tu." Pengine mtu mrefu atahisi anastahili kulipwa zaidi na aseme: "Hapana nahitaji elfu 10 zaidi."

Ushawahi kuingia katika ukumbi ukahisi unakaguliwa na kupuuzwa katika muda usiozidi sekundi kadhaa?

Watu wafupi wanalifahamu hilo vizuri sana.

Mwanamume mrefu anaposimama na kujitetea anaonekana kujiamiani, lakini kwa mtu wa urefu wangu anayepigania kusikika huonekana kama mtu asiyejiamini anyehitaji usaidizi.

Soma mengi


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved