logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Unajua jinsi nakupenda,'Diamond asherehekea siku ya kuzaliwa na ndugu yake Romy Jons

Bali na kazi yake msanii huyo anapenda familia yake, na kuitambua.

image
na Radio Jambo

Habari16 August 2021 - 12:54

Muhtasari


  • Diamond asherehekea siku ya kuzaliwa na ndugu yake Romy Jons

Bila shaka msanii na staa wa bongo Diamond Platnumz ni mfalme wa nyimbo zabongo flava Afrika mashariki.

Bali na kazi yake msanii huyo anapenda familia yake, na kuitambua.

Kwa muda sasa Diamond amekuwa akiongoza, na kuwa na wafuasi wengi kwenye vibao vyake vya hivi juzi.

Je kuna msanii ambaye anaweza vunja rekodi ya msanii huyo?Pia ni mkurugenzi mkuu wa lebo ya muziki ya Wasafi.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram alipakia picha ya zamani yake na ndugu yake Rommy huku akimtakia siku njema akisherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Kutokana na picha hizo ni wazi kwamba wawili hao walikuwa na uhusiano wa karibu sana nyakati zao za utotoni.

Pia alimwambia kwamba anafahamu jinsi anampenda.

Huu hapa ujumbe wake;

"Unajua jinsi ninavyokupenda ndugu yangu @romyjons," Aliandika Diamond.

Hizi hapa baadhi ya jumbe za mashabiki

_esmaplatnumz: WADOGO ZANGU πŸ‘©β€πŸ‘¦β€πŸ‘¦

iam_akujumbosso: @diamondplatnumz namwona nasib jrπŸ˜‚

wakuzoza: wa2 wanatoka mbali asee simba

vannnesamdeefunpage: mapacha toka zamani

swerry_bby: Du ulikua mtundu inaonekanπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

evans_wangunda: Happy birthday brothers πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯❀️❀️

victor_good_son: So mchezo mbali Sana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logoΒ© Radio Jambo 2024. All rights reserved