logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nitaoa kwa wakati ufaao,'Mwanahabari Trevor Ombija azungumzia kuoa

Pia alifichua kuwa kwa sasa hana haraka ya kuoa, lakini anatarajia kufanya hivyo wakati mzuri utakapofika.

image
na Radio Jambo

Habari23 August 2021 - 10:18

Muhtasari


  • Mwanahabari a runinga ya Citizen Trevor Ombija ni miongoni mwa wanahabari ambao wana talanta ya kazi yao
  • Ombija anafahamika sana kwa kazi yake, na vile anaishi maisha yake

Mwanahabari a runinga ya Citizen Trevor Ombija ni miongoni mwa wanahabari ambao wana talanta ya kazi yao.

Ombija anafahamika sana kwa kazi yake, na vile anaishi maisha yake.

Akizungumza na Kalondu Musyimi, Ombija alisema kwamba  yeye ni muumini wa ndoa na anajua kuwa inaweza kufanya kazi wakati wote ikiwa wenzi wote wako ndani ya hiyo ndoa.

"Ni juhudi za makusudi kutoka kwa nyinyi wawili, nyinyi wawili mnapaswa kuwa tayari kukubaliana, kuzungumza, ina kazi nyingi.

Haipaswi kuwa mtu mmoja anaweka asilimia ya 40% na mwingine  asilimia ya 60%, ninyi nyote mnapaswa kuwa 50-50. Maelewano ndio jambo kubwa katika ndoa, "Alieleza Ombija.

Pia alifichua kuwa kwa sasa hana haraka ya kuoa, lakini anatarajia kufanya hivyo wakati mzuri utakapofika.

"Nitafanya hivyo, kwa wakati unaofaa, na mtu sahihi. Muniombee!"

Ombija alifichua pia kwamba DM yake imejaa wanawake ambao ni warembi bali anawajibu yuko sawa.

Alizungumia uhusiano aliokuwa nao miaka 10 iliyopita, na hata kulipa mahari lakini mambo hayakuenda sawa.

Je unaweza pata mwanamume mwanifu kweli, ambaye anatumiwa jumbe na wanwake lakini anawapuuza?

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved