logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwili wa mwanamke aliyetoweka wapatikana umezikwa katika boma la jirani yake

Familia ya mwanamke huyo ilisema alitoweka Septemba mwaka jana.

image
na Radio Jambo

Habari13 March 2023 - 09:53

Muhtasari


• Familia ya mwanamke huyo ilisema walipiga ripoti kuhusu kupotea kwake, watuhumiwa wakashikwa lakini baadae kuachiliwa huru.

• Mwili huo ulifukuliwa kikamilifu na kupelekwa katika hospitali ya Kakamega kwa uchunguzi wa kina.

Polisi katika kaunti ya Kakamega wanachunguza kisa cha ajabu ambapo mwanamke aliyeripotiwa kutoweka miezi michache iliyopita kupatikana amezikwa katika boma la jirani yake.

Kulingana na taarifa moja runingani Citizen, kisa hicho kiliripotiwa kutokea katika eneobunge la Ikolomani kaunti ya Kakamega ambapo mwili huo ulipatikana na mwanamume mmoja aliyekuwa akichimba udongo kwa ajili ya matumizi kwa nyumba yake mpya kabla ya kuupata mwili huo.

Fabian Muteshi, mkaazi wa Kitengela alisafiri kwenda nyumbani kwao Ikolomani kwa ajili ya ujenzi wa nyumba yake, katika harakati za kuchimba mchanga, alifikia mabaki ya mwili wa mtu ambayo yalidhaniwa kuwa ya mwanamke huyo aliyeripotiwa kutoweka.

"Nilikuwa nikivuna udongo wa udongo kwa ajili ya nyumba yangu mpya ninayojenga, ndipo nilipokuta fuvu la kichwa cha binadamu likiwa na viungo vingine vya mwili. Sijawahi kuogopa hivyo," Muteshi aliiambia Citizen.

Familia moja ilijitokeza na kuutambua mwili huo kuwa wa mpendwa wao Rosa Kamoya, mwenye umri wa miaka 37 aliyeripotiwa kutoweka nyumbani kwa njia za utata mwezi Septemba mwaka jana.

Baba yake marehemu huyo alisema kwamba bintiye alitoweka mwaka jana akiwa na dada zake wawili katika kijiji jirani na tangu siku hiyo juhudi za kumtafuta zimeambulia patupu kwa Zaidi ya miezi 7 sasa.

Mwili huo ulifukuliwa kutoka hapo na kupelekwa katik hospitali ya Kakamega ukisubiri uchunguzi Zaidi wa maiti.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved