logo

NOW ON AIR

Listen in Live

CS Muturi: Siwezi kujiuzulu kutoka kwa serikali sababu nilishiriki kikamilifu kwenye kampeni!

Katika mazungumzo hayo, Muturi aliweka wazi kwamba tangu aonekane kuanza kuipinga serikali anayoihudumua, hajawahi hudhuria kikao chochote cha baraza la mawaziri, ikiwemo kikao cha juzi

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari13 March 2025 - 08:47

Muhtasari


  • Waziri huyo alisisitiza kwamba uamuzi wa chama ulifanywa na wakuu ndani ya chama hicho, akisema kwamba hakuna mwingilio wowote kutoka upande wake.
  • Muturi amekuwa akionekana kuipinga serikali anayoihudumia haswa baada ya mwanawe kuwa miongoni mwa waliotekwa nyara na vyombo vya dola wakati wa kilele cha maandamano ya Gen Z mwaka jana.

Justin Muturi asisisitiza kwa nini hana mpango wa kujiuzulu

WAZIRI wa utumishi wa umma, Justin Muturi ametaja sababu ambayo inamfanya hawezi hata kidogo kuwa na fikira za kujiuzulu kutoka kwa serikali ya Kenya Kwanza.

Akizungumza Jumatano katika kikao cha JKL kwenye runinga ya Citizen, Muturi ambaye amekuwa mwiba Mchungu kwenye kitovu cha serikali inayoongozwa na rais William Ruto alisisitiza kwamba hana mpango wa kujiuzulu.

Spika huyo wa zamani alisema kwamba ameketi kikato katika serikali ya Kenya kwanza nah ana mpango wa kujiuzulu kwa kuwa alishiriki kikamilifu katika kampeni za uchaguzi mkuu 2022 kumpigia debe Ruto kuwa rais.

“Mimi bado niko kwa serikali kwa sababu kama mnavyojua bado niko kwenye ule muungano na pili ni kwamba nilishiriki kikamilifu katika kampeni za Kenya Kwanza kuelekea uchaguzi mkuu wa 2022. Na hivyo niko kikamilifu katika haki zangu za kimuungano kuwa ndani ya serikali,” Muturi alisema.

Kuhusu chama cha DP ambacho alikuwa anakiongoza kabla ya kuteuliwa kama mwanasheria mkuu na baadae Waziri wa utumishi wa umma, kuandika barua rasmi wakitaka kujiondoa katika serikali, Muturi alisema kwamba huo ni uamuzi wa chama nah ana mkono katika uamuzi huo.

Muturi aliweka wazi kwamba kabla ya kuteuliwa kutumikia serikali ya Kenya Kwanza, alijiuzulu kama mwenyekiti wa chama hicho na kwamba barua ya kutaka kujiondoa kwenye Kenya Kwanza aliiona tu kama Mkenya mwingine yeyote.

Waziri huyo alisisitiza kwamba uamuzi wa chama ulifanywa na wakuu ndani ya chama hicho, akisema kwamba hakuna mwingilio wowote kutoka upande wake.

Muturi amekuwa akionekana kuipinga serikali anayoihudumia haswa baada ya mwanawe kuwa miongoni mwa waliotekwa nyara na vyombo vya dola wakati wa kilele cha maandamano ya Gen Z mwaka jana.

Mara si moja, Waziri huyo ameitisha mikutano na vyombo vya Habari kukashifu jinsi baadhi ya idara za serikali haswa katika masuala ya usalama zinavyoendeshwa, akilaani vikali ongezeko la utekaji nyara na kamata-kamata ambazo zimekuwa zikiendeshwa na maafisa wa usalama.

Katika mazungumzo hayo, Muturi aliweka wazi kwamba tangu aonekane kuanza kuipinga serikali anayoihudumua, hajawahi hudhuria kikao chochote cha baraza la mawaziri, ikiwemo kikao cha juzi kilichofanyika katika ikulu ya Nairobi.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved