logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Warusi kuruhusiwa kutuma dola 10,000 pekee nje ya taifa hilo

Warusi sasa wataruhusiwa kutuma kiasi cha dola 10,000 pekee nje ya taifa hilo.

image
na

Dakia-udaku03 March 2022 - 06:44

Muhtasari


• Serikali ya Urusi sasa imetangaza kiwango kipya cha pesa ambacho Mtu anaweza kutuma nje ya taifa hilo.

• Kwa raia wa Urusi kuanzia sasa hawatoruhusiwa kutuma nje ya Nchi zaidi ya dola 10000 na wasio wananchi wa Urusi  hawatoruhusiwa kutuma nje ya Nchi, dola 5000 .

 

KWA HISANI

Katika jitihada za kupambana na vikwazo vya kiuchumi vilivyowekwa dhidi yake na Mataifa mbalimbali, Serikali ya Urusi sasa imetangaza kiwango kipya cha pesa ambacho Mtu anaweza kutuma nje ya taifa hilo.

Kwa raia wa Urusi kuanzia sasa hawatoruhusiwa kutuma nje ya Nchi zaidi ya dola 10000 na wasio wananchi wa Urusi  hawatoruhusiwa kutuma nje ya Nchi, dola 5000 .

Hali hii inatarajiwa kuibua kipindi kigumu kwa wafanyiashara wa Urusi ambao wamewekeza katika mataifa ya nje na sasa watalazimika kutafuta mbinu mbadala ili kuhakikisha mambo yao yanaendelea vizuri.

Hatua hii inalenga kuzuia mataifa mbalimbali kufaidi kutokana na uchumi wa Urusi kipindi hiki wanazidi kusukuma vita vya kijeshi dhidi ya taifa la Ukraine.

Ifahamike kwamba siku chache zilizopita, kampuni mbalimbali zilisitisha huduma zao nchini Urusi kwa kile walichokitaja kama kutokuwepo kwa mazingira mazuri ya kufanyia kazi.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved