
Polisi walianzisha msako mkali kufuatia msururu wa wizi katika Barabara kuu ya Thika mnamo Machi 11,2025 baada ya kundi la vijana kuvamia magari na wasafiri baada ya mkutano wa Rais Ruto.
Katika taarifa iliyosomwa Alhamisi Machi 13,2025 kutoka kwa idara ya upelelezi wa makosa ya Jinai DCI ilidhibitisha kuwa angalau watu wanane walikamatwa kutokana na tukio hilo.
‘Kwa kujibu madai na tetesi kutokana na matukio ya uvamizi na wizi yaliyotekelezwa na watu
waliolenga watu wasio na hatia katika Barabara kuu ya Thika mnamo Machi 11,2025 , Maafisa wa polisi wameanzisha uchunguzi
wa kuwatambua wahalifu hao wote waliosababisha vitendo hivyo vyote vya
uchama’ DCI ilieleza.
DCI iliweza kumtambua mshukiwa mmoja kwa Jina Junior Odinga
aliyekuwa amejihami kwa kisu alipovamia raia
mmoja na kumuibia simu aina ya Oppo A77S
iliyotoka shilingi elifu ishirini na nane 28,000.
‘’Oginga alikamatwa katika Barabara kuu ya Thika na kupelekwa katika kituo cha polisi cha Pangani taarifa ilieleza''.
Washukiwa wengine saba waliweza kukamatwa kutokana na
msako mkali ulioendeshwa na maafisa wa polisi, waliokamatwa ni Jared Nyanza,Darlin
Lande,Daniel Okombe,Mike Robert,Elvis Otieno,Reagan Omondi na Mathenge Gathiri
hao walikamatwa kwa kuwaibia wapita njia katika eneo la Mathare mtaa wa 4( Mathare
Area 4).
Washukiwa hao waliweza kupelekwa katika kituo cha polisi cha
Muthaiga DCI ilieleza.Polisi waliweza kupata shati saba mpya ambazo zilikisiwa
ziliibiwa kutoka kwa waathiriwa,DCI ilieleza kuwa washukiwa wote waliweza
kukamatwa na kufikishwa katika vituo vya polisi ili kuandikisha taarifa.
Pikipiki nyingi zilionekana siku ya Jumanne Adhuhuri zilizowashutua
wasafiri na watumizi wa Barabara kwa kusababisha hali ya wasiwasi na
sintofahamu miongoni mwa wananchi.
Katika Video zilizoonekana katika mitandao ya kijamii zilionyesha vijana wengi
wakifunga sehemu za Barabara, kuwalazimisha wapitanjia kuwapa walivyokuwa
wamebeba Pamoja na kuwaibia waliokuwa ndani ya magari ya binafsi.
Walekwa wa matukio hayo walipata wakati mgumu kuweza kujinasua kutoka kwa wahuni hao huku tahadhari ya kutotumia Barabara hiyo ikisambazwa mitandaoni kuwaonya wananchi kutotumia Barabara hiyo.
‘’Kwa sasa wasafiri muepuke kutumia Barabara kuu ya Thika katika mpitio wa Barabara ya wasafiri
wa miguu ya KCA kuna kundi la Vijana
amabalo linawaibia watu na hata kuingia kwenye magari ya umma Huduma ya polisi
kwa umma tunataka usaidizi wenu maelezo
kutoka kwa Sikika Usalama Kwa Barabara(Sikika Road Safety) yalichapishwa katika
ukurasa wao wa Facebook mnamo Machi 11,2025’’.