logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Shirika Plan: Rais Ruto azindua mpango maluum kwa ajili ya wakimbizi nchini

Ni mpango maalum ambao unalenga kuwasaidia na kuwakubali wakimbizi katika jamii pana ya Wakenya ili kuweza kutambuliwa na kuheshimiwa sana katika taifa.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri28 March 2025 - 16:38

Muhtasari


  • Ni mpango maalum ambao unalenga kuwasaidia na kuwakubali wakimbizi katika jamii pana ya Wakenya ili kuweza kutambuliwa na kuheshimiwa sana katika taifa.
  • Kenya ilianzisha pango wa kuwakaribisha wakimbizi nchini mnamo mwaka wa 1980 kutoka kwa mataifa jirani kutokana na vita katika mataifa yao,mnamo mwaka wa 1991 hadi 1992 Kenya iliweza kuwapokea wakimbizi kutoka taifa la Somalia.

Rais Willam Ruto amezindua mpango maalum unaojulikana kama shirika plan kwa ajili ya Wakimbizi nchini.

Ni mpango maalum ambao unalenga kuwasaidia na kuwakubali wakimbizi katika jamii pana ya Wakenya ili kuweza kutambuliwa na kuheshimiwa sana katika taifa.

Kenya ilianzisha mpango wa kuwakaribisha wakimbizi nchini mnamo mwaka wa 1980 kutoka kwa mataifa jirani kutokana na vita katika mataifa yao.

Mnamo mwaka wa 1991 hadi 1992 Kenya iliweza kuwapokea wakimbizi kutoka taifa la Somalia.

Taifa la Kenya  lina Kambi mbili kuu za kuweza kuwahifanyi na kuwapokea wakimbizi wa ndani kwa ndani au kutoka nje ya mataifa mengine kambi ya Daadab na kambi ya Kakuma.

Kuna kambi ya Daadab ambayo ilianzishwa mwaka wa 1991 ambayo iliweza kuwapokea wakimbizi zaidi ya 420,000 kutoka taifa la Somalia kutokana na kuzuka kwa vita katika taifa hilo la Somalia ambapo kulizuka machafuko ya vita kati ya serikali ikiongozwa na Syyad Bare na waasi mwaka wa  1992.

Mnamo mwaka wa 2011 taifa la Kenya liliweza kupokea wakimbizi wengine 130,000 kutoka taifa la Sudan Kusini hio ni kutokana na machafuko ya vita vikali  vilivyoshuhudiwa kati ya rais Salvakir na Riek Machari ambapo watu wengi waliweza kuuwawa na wengine kupoteza  makao  hivyo kukimbilia mataifa jirani kwa ajili ya usalama wao.

Kenya Pia ina kambi nyingine ya Wakimbizi ambayo inaitwa Kakuma ambayo mara nyingi hupokea wakimbizi kutoka taifa la  Uhabeshi( Ethiopia)

Kenya imekuwa mshiriki mkuu wa kupokea na kuwasaidia wakimbizi kwa kile ambacho kinaonekana kuwa ni taifa lenye amani  na lenye sheria na mikakati bainifiu ya kuhakikisha kuwa usalama wa wakimbizi unazingatiwa ipasavyo kwa ajili ya  kuwa kwa amani na umoja.

Kenya huweza kuwapokea wakimbizi kutoka mataifa ya  Somalia, Sudan, Demokrasia ya  Kongona na  taifa la Burundii.

Chini ya kifuchiu  cha sheria  cha  mwaka wa 2011 sheria hiyo imewapa uhuru wa makao  na kuishi katika taifa la kenya kwa kupata haki zote za kimsingi na kuweza kujumuika kama  raia wengine  na kupata haki  za kimsingi kutoka  katika taifa  la Kenya.

 Kwa hivyo rais kuanzisha mchakato huo ni njia mojawapo ya kuhakikisha kuwa wakimbizi wanaishi  kama wakenya wengine na kufaidi kwa miradi ya serikali na hata  vilevile kuweza kukaribisha misaada kutoka kwa mataifa  mengine ambayo yana ari ya kusaidia kukuza umoja na ubinadamu.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved