logo

NOW ON AIR

Listen in Live

William Ruto sio rais sahihi kwa taifa la Kenya - Justin Muturi

Justin Mutruri sasa anasema kwamba rais William Ruto sio rais sahihi kwa taifa la Kenya.

image
na Japheth Nyongesa

Yanayojiri04 April 2025 - 12:13

Muhtasari


  • "Unaambiwa uende uweke sahihi kwa mkataba ukiwa kwa uwanja wa ndege, na ni rais anakupigia. Ni jambo la kushangaza sana kwamba tuko na Wiliam Ruto kama rais wa wa taifa la Kenya," alisema spika huyo wa zamani.
President William Ruto and Former Public Service CS Justin Muturi /FILE
Aliyekuwa waziri wa Utumishi wa umma, Justin Mutruri sasa anasema kwamba rais William Ruto sio rais sahihi kwa taifa la Kenya. Muturi kwenye kikao na waandishi wa habari amemtaja rais kama mwenye upungufu mwingi sana.

Akizungumza kwenye kituo kimoja cha redio humu nchini, Muturi aliendelea na kuleza kwamba rais Ruto ni mtu asiyeeleweka na ni watu wawili tofauti.

"Nadhani William Ruto ni mtu aina mbili tofauti, Ruto ambaye anaonekana kwa umma ni tofauti sana na yule anayekaa kwenye ikulu ya rais na kuifanya maamuzi. Na mtu kama huyo ni hatari. Nadhani kwamba william Ruto sio sahihi kuwa rais wa Kenya," alisema Mutruri.

"Hilo ndilo hitimisho langu na sina chuki na yeye, Nikiona rais akizungumza kwenye kikao cha mawaziri na anasema hataki kuona ufisadI kwa seriksali yake. Nashangaa huyu ni nani anaongea... yeye ni kiongozi wa ufisadi," aliendelea.

Waziri huyo wa zamani ameendelea na kueleza kuhusu mkataba wa Adani ambao walikuwa wamepewa idhini ya kumiliki uwanja wa ndege. Amesisitiza kwamba hakuna mkataba wa serikali ambao rais hufanya bila kufikiria atakachokipata yeye.

"Yeye ndie alikua nyuma ya Adani, Mshauri wake Adan Muhamed alinialika kwa mkutano na nikajua kila kitu kuhusu mpango huo. Ruto akija na shughuli yeyote inahusu kuunda pesa. Kuna wakati waliniletea mkataba wa MOU, kutoka wizara ya mazingira.  Ilikuwa 1M US Dollars na wanataka hiyo pesa ipelekwe  moja kwa moja kwa wizara ya mazingira bila kupitia hazina ya kitaifa,"  alieleza zaidi.

"Unaambiwa uende uweke sahihi kwa mkataba ukiwa kwa uwanja wa ndege, na ni rais anakupigia. Ni jambo la kushangaza sana kwamba tuko na Wiliam Ruto kama rais wa wa taifa la Kenya," alisema spika huyo wa zamani.

Rais Wlilliam Ruto alimfuta Muturi kazi huku akimtaja kama mtu asielewa kazi yake katika wizara zote mbili ambozo amefanya chini yake katika serikali ya Wlilliam Ruto.

 "Nilikuwa na tatizo na Mwanasheria Mkuu aliyekuwepo hapo awali—alikuwa hana uwezo. Lakini sasa, nina mtu mwenye uwezo mkubwa katika nafasi hiyo, na nina hakika masuala ya Waqf yatatatuliwa ndani ya miezi michache," alisema Ruto.

Muturi hakusita kujibu tuhuma hizo, akisema kuwa madai ya Ruto hayakuwa ya kweli. Alieleza kuwa Sheria ya Waqf Na. 8 ya 2022 haielekezi kuanzishwa kwa "Mfuko wa Waqf wa Kiislamu" na kuongeza kuwa waqf ni mali ya hisani inayosimamiwa na Tume ya Waqf.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved