logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Obidan Dela: Hii Ndio Sababu Najiita Mume Wa Wajane, Ma’shosho Na Single Moms

“Mimi ndio nilikuwa mtu wa kwanza kuleta shosho wa Chira TikTok. Watu walikuwa wananiita ‘kijana wa shosho’ kwa sababu ya kusimama na yeye.”

image
na MOSES SAGWE

Burudani26 February 2025 - 12:04

Muhtasari


  • Alisisitiza kwamba watu kumuita mume wa wajane ni ishara ya kusifia jinsi anavyowasaidia watu wasiojiweza.
  • TikToker huyo pia aliweza kuzungumzia kuhusu uhusiano wake na Esther, nyanya yake aliyekuwa TikToker Brian Chira.

Obidan Dela na shosho wa chira

TIKTOKER Obidan Dela kwa mara ya kwanza amefunguka kwa nini anajitambua kama mume wa wanawake waliofiwa na waume zao, wale walioachwa na baba watoto wao na kina ajuza.

Akizungumza kwenye podikasti ya Mwende Macharia, Dela alisema kwamba aliamua kukumbatia jina hilo baada ya TikTokers wenzake kuanza kumuita hivyo kimchezo.

Kwa mujibu wa Dela, aliona kujiita ‘mume wa waja, bibi na mama wasio na waume’ si vibaya kwani pia aligundua wengi wa watu ambao walikuwa wanamlilia kwa misaada ya kila aina ni watu kutoka matabaka hayo matatu.

“Mimi ni mume wa wajane, single moms na pia bwana wa ajuza wote. Na hii ilikuja kutoka kwao kwa sababu mimi ndio hutoa jukwaa pekee la kuwasaidia watu kwenye TikTok. Sasa hivi hata usikie kama uko na shida umefungiwa nyumba, ukija kwa Obidan Dela utapata msaada,” alisema.

Alisisitiza kwamba watu kumuita mume wa wajane ni ishara ya kusifia jinsi anavyowasaidia watu wasiojiweza.

“Kwangu mimi wakiniita mume wa wajane ni njia ya kuni’appreciate. Mimi ndiye mtu pekee ambaye naweza ingia TikTok Live nikose kujisaidia na nisaidie watu. Mimi huwa sifanyi mzaha TikTok,” Dela alisema huku akitetea kusaidia kwake watu kutokana na yale maisha ambayo alikulia.

TikToker huyo pia aliweza kuzungumzia kuhusu uhusiano wake na Esther, nyanya yake aliyekuwa TikToker Brian Chira.

Dela alisema kwamba anampenda sana ‘shosho wa Chira’ huku akitetea jinsi alimpeleka katika mgahawa ghali siku ya wapendanao kufurahisha maisha.

“Mimi ndio nilikuwa mtu wa kwanza kuleta shosho wa Chira TikTok. Watu walikuwa wananiita ‘kijana wa shosho’ kwa sababu ya kusimama na yeye.”

“Mimi na Shosho wa Chira ni mapenzi tu, unajua tunafanya out of love. Shosho anastahili kupendwa kwa sababu hujawahi pendwa. Hata ile kumpeleka mgahawani afurahie Valentine ilikuwa ni surprise sana. Unajua hujawahi nunuliwa nguo…unajua kitu kimoja kimoja kuhusu Valentine ni kwamba si lazima umpende mtu ndio umfanyie kitu, unaweza surprise mzazi wako…ni mwezi wa mapenzi na unaweza onyesha mapenzi hata kwa mbwa wako, jirani, kakako…hiyo ndio maana ya Valentine,” Dela alitetea uhusiano wake na Shosho.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved