logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Charlie Jones, Kijana Gen Z alaumu pombe kwa uvumi wa kuachana na Betty Kyallo, aomba radhi

Licha ya kutofunga harusi katika ndoa rasmi, kijana huyo alimrejelea Betty Kyallo kama mke wake akisema kwamba anamjua kama mtu muelewa ambaye atamsamehe.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani14 March 2025 - 12:00

Muhtasari


  • Kwa zaidi ya mwaka mmoja wamekuwa wakionyesha mapenzi yao hadharani, na kuamua kuacha kufuatiliana kwenye mitandao ya kijamii.
  • Awali, walikuwa wakifuatana kwenye akaunti zao kubwa za Instagram na mara kwa mara walichapisha picha na video wakiwa pamoja. 

Betty Kyallo na Charlie Jones

CHARLIE Jones, kijana mdogo ambaye amekuwa akitajwa kuwa mpenzi wa malkia wa runingani, Betty Kyallo amejitokeza waziwazi kuzungumzia tetesi za penzi lao kuvunjika.

Kupitia Instagram, Jones alichapisha jumbe zenye aya ndefu akionekana kukanusha vikali uvumi wa kuachana kwake na Betty Kyallo.

Hata hivyo, katika utetezi wake kwamba penzi lao bado lingali hai, kijana huyo alionekana kulaumu pombe kwa kauli za awali, akiweka wazi kwamba hatua yake itakayofuata ni kumuomba Kyallo samahani.

Licha ya kutofunga harusi katika ndoa rasmi, kijana huyo alimrejelea Betty Kyallo kama mke wake akisema kwamba anamjua kama mtu muelewa ambaye atamsamehe.

“Hakuna mtu ameachwa, hiyo ilikuwa ni pombe inazungumza. Ninampenda sana mke wangu na sasa naenda kumuomba msamaha. Kutoka kwa vitendo vyangu, mimi ndiye ninastahili kuachwa na sio vinginevyo,” Jones alisema.

“Tulijenga haya mahusiano na nyinyi wajinga mnadhani kwamba huu ndio wakati ambapo mnampa mke wangu ushauri. Wanawake wenye majungu wanampigia simu wakimuambie eti ‘mrembo unstahili mazuri’,” Jones alimaliza huku akitamka neno la nguoni.

Uvumi wa kuachana kwao ulifichuka mapema Alhamisi baada ya wadadisi wa mitandaoni kubaini kwamba wawili hao walikuwa wamesitisha urafiki wao kupitia kurasa za Instagram.

Kwa zaidi ya mwaka mmoja wamekuwa wakionyesha mapenzi yao hadharani, na kuamua kuacha kufuatiliana kwenye mitandao ya kijamii.

Awali, walikuwa wakifuatana kwenye akaunti zao kubwa za Instagram na mara kwa mara walichapisha picha na video wakiwa pamoja. Hata hivyo, hatua yao ya hivi karibuni imeacha wengi wakijiuliza iwapo uhusiano wao uko shakani.

Kijana huyo mwenyewe ndiye aliyeanzisha uvumi huo kwa msururu wa jumbe kwenye Instagram ambazo sasa ameonekana kujutia.

"Ndio, tumeachana. Hata akiniaibisha, sitadanganya kuhusu jina lake. Aseme anavyotaka," aliandika.

Akaongeza: "Usiseme uongo kunihusu, nami sitasema ukweli kukuhusu."

Charlie pia alipakia meme ikionyesha kuwa anajitambua kwamba yeye sio mzuri kabisa na hajali jinsi anavyochukuliwa na watu.

Katika chapisho lingine, alizungumzia afya ya akili ya wanaume, akieleza kuwa mara nyingi haizingatiwi hadi mambo yanapozidi kuwa mabaya.

"Hakuna anayejali afya ya akili ya mwanaume hadi hasira itokee, ndipo kila mtu anaanza kumwona kama mtu mbaya," ilisomeka meme hiyo.

Hata hivyo, katika muda wote huu, Betty Kyallo amesalia kimya asiweze kuzungumzia suala hilo.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved