logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baba Talisha: Haya ndio nimejifunza tangu kifo cha Brian Chira mwaka jana

Brian Chira aliaga dunia Machi 16 mwaka uliopita katika kile kilichoripotiwa na polisi kama ajali ya kugongwa na gari barabarani.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani17 March 2025 - 11:19

Muhtasari


  • Brian Chira aliaga dunia Machi 16 mwaka uliopita katika kile kilichoripotiwa na polisi kama ajali ya kugongwa na gari barabarani.

Brian Chira na Baba Talisha//MAKTABA

FAUSTINE Lipuku Lukale, mpiga picha ambaye aliibuka kuwa rafiki wa kipekee aliyesimama na familia ya TikToker Brian Chira wakati wa kifo chake amefunguka yale aliyojifunza wakati na baada ya kifo hicho.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Lukale ambaye wengi wanamfahamu kama Baba Talisha aliungana na mamia ya mashabiki wengine wa marehemu Brian Chira kuadhimisha kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kufa kwake katika ajali.

Alisema kwamba tangu kifo cha rafiki huyo, amejifunza mambo mawili makuu, yote yakionekana kurejelea mishale aliyotupiwa baada ya kusimama na familia yake katika mazishi.

Baba Talisha ambaye aliburuzana na nyanyake Brian Chira siku chache tu baada ya kuongoza TikTokers wenzake kuchangisha zaidi ya shilingi milioni 8 kwa ajili ya mazishi ya Chira, alisema kwamba hajutii hata kidogo fadhila alizoonyesha.

“Mwaka umepita na Leo inanikumbusha mambo 2 tangu Huyu Kijana Chira aondoke.

1. Usijutie fadhili ulizoonyesha mtu ambaye hakustahili. Walikukosea, ukawatendea mema, na kwa ajili hiyo unapaswa kujivuna.

2. Siku moja, mtu uliyejitolea sana kwa ajili yake atageuka na kusema hakuwahi kuomba, na itaumiza kwa sababu watakuwa sahihi,” Baba Talisha alisema.

Brian Chira aliaga dunia Machi 16 mwaka uliopita katika kile kilichoripotiwa na polisi kama ajali ya kugongwa na gari barabarani.

Jumamosi, TikToker mwenzake ambaye mpaka sasa amesalia kuwa msaada wa pekee kwa nyanyake Brian Chira, Obidan Dela alitembelea familia hiyo na kurekodi video wakiadhimisha mwaka mmoja tangu kifo cha mpenzwa wao.

Katika video hiyo, Obidan Dela na Watoto hao walikuwa wameishikilia picha kubwa ya Brian Chira huku wakikumbuka na kukariri kauli aliyopenda kuitamka ‘kama wewe si pesa huwezi nipa stress’.

Pia waliimba kwa huzuni wimbo wa Otile Brown ‘One Call’ ambao ulisheheni sana wakati wa mazishi ya Chira ambapo ilisemekana ulikuwa moja ya nyimbo alizozipenda pakubwa.

“Yo guys, Obidan Dela hapa, guys, na niko na Brian Chira na Sophie Njeri Chira Kadogo na wananiambia kama vile Chira alikuwa anawaambia, ‘Kama wewe si pesa, huwezi ni-stress.’”

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved