logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Georgina Njenga: Huwa najuta kuachana na Tyler Mbaya kwa sababu mitaani kuna baridi

“Kusema ukweli kuna wakati mwingine mimi hujuta kuondoka. Kwa sababu mitaani kuna baridi. Lakini majuto ni kama 2%,” Njenga aliongeza.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani26 March 2025 - 12:16

Muhtasari


  • Georgina Njenga alikiri kwamba kuna wakati huwa anakaa chini ya kujuta kuvunja uhusiano wake na baba wa mwanawe, akitania kwamba mitaani kuna baridi sana.
  • “Tuliachana miaka miwili iliyopita, inaelekea miaka 2 ikifika Mei. Kilichoniuma zaidi ni kuvunjika kwa familia, ikilinganishwa na kuvunjika kwa penzi,” alisema.

Georgina Njenga

GEORGINA Njenga amevunja kimya chake kuhusu kuvunjika kwa uhusiano wake na aliyekuwa mpenzi wake, Tyler Mbaya maarufu Baha Machachari.

Akizungumza kwenye podkasti ya Morin Actress, Njenga alifichua kwamba ifikapo Mei mwaka huu, watamaliza miaka 2 tangu kuachana kwao.

Mama huyo wa binti mmoja alipoulizwa kuhusu chanzo cha kusambaratika kwa huba lao na kumweka binti yao njia panda kukosa penzi la mzazi mmoja kati yao, alisema kwamba baada ya kutathmini kwa muda, wakati mwingine anahisi haikufaa kuwa sababu kubwa ya kusababisha kuachana kwao.

Georgina Njenga alikiri kwamba kuna wakati huwa anakaa chini ya kujuta kuvunja uhusiano wake na baba wa mwanawe, akitania kwamba mitaani kuna baridi sana.

“Tuliachana miaka miwili iliyopita, inaelekea miaka 2 ikifika Mei. Kilichoniuma zaidi ni kuvunjika kwa familia, ikilinganishwa na kuvunjika kwa penzi,” alisema.

“Hata haikuwa sababu ya msingi sana, nilikuja kuifikiria (baadae) ni kama ilikuwa ya msingi kidogo lakini kwa sasa kusema ukweli kuna wakati mwingine mimi hujuta kuondoka. Kwa sababu mitaani kuna baridi. Lakini majuto ni kama 2%,” Njenga aliongeza.

Kuhusu kilichomuuma zaidi katika harakati ya kutengana kwake na Tyler Mbaya, Georgina Njenga alisema kwamba aliumia zaidi kuona familia ikisambaratika kuliko kuona penzi likimwagika.

“Nilikuwa nakaa tu hivi najiambia kwamba nilikua bila baba na hapa binti yangu nitamuona akikua bila baba… lakini pia nilikuwa najijibu kwamba siwezi teseka kwa sababu ya mtu (mtoto) ambaye atakua na aondoke kuishi maisha yake aniwache,” Njenga alisema.

Hata hivyo, alisema kuwa majuto hayo yanakuja kwake kwa njia nyepesi kwani huwa anafikiria kwamba akitathmini jinsi alivyoondoka, pengine angepewa nafasi ya kufanya maamuzi upya angeshughulikia suala hilo kwa njia tofauti.

Ingawa uhusiano wao haukufanikiwa, Georgina alikiri kwamba uzazi wa ushirikiano umeboreka baada ya muda.

Alimsifu mama yake kwa kuchukua jukumu muhimu katika kumlea binti yao na kuwezesha mawasiliano kati yake na Baha.

Akieleza kwamba kwa vile Baha mara nyingi huzungumza na mama yake, kuna haja ndogo ya mawasiliano ya moja kwa moja kati yao.

Georgina na Baha walikuwa mmoja wa wanandoa wachanga waliopendwa sana nchini Kenya, lakini walitengana mwaka wa 2023, miezi michache tu baada ya kumkaribisha binti yao.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved