logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mrembo alisha halaiki akisherehekea kuwa mtu wa kwanza kupanda ndege kutoka Kijiji chake

Katika video hiyo, mrembo huyo alibandika bango kubwa lenye ujumbe ‘mtu wa kwanza kutoka Kijiji chetu kupanda ndege’ kando ya viti na maturubai wakiwa wamefurika watu kujivinjari kwa sherehe.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani08 April 2025 - 10:05

Muhtasari


  • Aliwaandalia mlo na kuwataka kujumuika naye kumsherehekea kwa kuweka rekodi hiyo adimu.
  • Tukio hilo liliwashangaza wengi, baadhi wakimhongera kwa rekodi hiyo na wengine wakimsuta kwa kuharibu hela katika kile walichokitaja kuwa jambo lisilo la maana.

Mwanamke afanya bonge la party

MWANAMKE mmoja mwenye umri wa makamo amezua gumzo katika mtandao wa TikTok baada ya kuandaa tafrija kubwa la kusherehekea kuweka rekodi ya kuwa mtu wa kwanza kutoka Kijiji chao kuairi ndege.

Katika video hiyo, mrembo huyo alibandika bango kubwa lenye ujumbe ‘mtu wa kwanza kutoka Kijiji chetu kupanda ndege’ kando ya viti na maturubai wakiwa wamefurika watu kujivinjari kwa sherehe.

Aliwaandalia mlo na kuwataka kujumuika naye kumsherehekea kwa kuweka rekodi hiyo adimu.

Tukio hilo liliwashangaza wengi, baadhi wakimhongera kwa rekodi hiyo na wengine wakimsuta kwa kuharibu hela katika kile walichokitaja kuwa jambo lisilo la maana.

Hata hivyo, wengi walionekana kukubaliana naye wakisema kuwa mtu anapoamua kusherehekea mafanikio yake japo madogo, aachwe tu asherehekee maana kwa wengine yanaweza yakaonekana ya kawaida tu lakini kwa mhusika ni makubwa na yenye thamani kubwa kwenye kumbukumbu ya maisha yake.

Tazama video hiyo hapa chini kisha utoe maoni yako;

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved