logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Esther Musila aomboleza kifo cha ‘mwanawe’ zaidi ya miaka 7 tangu vifo vya wazazi wake

Musila alifichua kwamba kijana huyo ambaye alikuwa ndio anajiandaa kujiunga chuo kikuu amefariki, takribani mwaka mmoja baada ya kuwazika wazazi wake wote.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani09 April 2025 - 11:15

Muhtasari


  • Musila alifichua kwamba kijana huyo ambaye alikuwa ndio anajiandaa kujiunga chuo kikuu amefariki, takribani  miaka saba baada ya kuwazika wazazi wake wote.
Esther Musila na wanawe

FAMILIA ya Esther Musila imetupwa kwenye kipindi cha maombolezo baada ya kufiwa na kijana ambaye amekuwa akimlea kama mwanawe.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Musila alisimulia kwa uchungu jinsi kifo kimeipokonya familia mtu wa maana ambaye alikuwa na asilimia kubwa ya maisha yake mbele yake.

Musila alifichua kwamba kijana huyo ambaye alikuwa ndio anajiandaa kujiunga na chuo kikuu amefariki, takribani miaka saba baada ya kuwazika wazazi wake wote.

“Kwa mwana ambaye nilimpenda kama wangu, hili limeniuma sana. Ni takribani mwaka mmoja tangu tuwazike wazazi wako, nilizungumza na wewe siku mbili zilizopita na Nilifurahia mipango yako ya kujiunga chuo kikuu na nilitegemea kukuona ukitimiza ndoto zako za kuwa mwanasayansi,” Musila aliomboleza.

Musila alikumbuka jinsi kijana huyo na mwanawe Glenn Naibei walikulia Pamoja kama kaka na dada wa tumbo moja tangu darasa la kwanza.

Musila alisema kwamba kando na kuhisi kupata pigo, amekasirika kwamba kijana huyo amefariki angali na umri mbichi kabisa kama jani la mgomba.

“Hukustahili kufa kwa jinsi hii, nina hasira. Baadhi yetu tulikufeli. Pumzika kwa amani mwanangu kwa maana sasa umeungana na wazazi wako ambao walikulea kwa nguvu zote wakati wa siku zao za mwisho duniani. Naamini walikuona ukitaabika na walikutaka uungane nao. Pumzika vizuri Malakwen,” Musila alimaliza.

Hata hivyo, hakuweka wazi kiini cha kifo cha kijana huyo licha ya kudokeza kwamba watu wake wa karibu, akiwemo yeye huenda walimfeli kwa njia Fulani kupelekea kifo chake.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved