logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nadhani wasichana wanaopata mimba wakiwa shuleni wanapaswa kuendelea na elimu-Akothee

Lakini wanachosahau wengi ni kuwa ujauzito sio ugonjwa wala virusi.

image
na Radio Jambo

Habari03 June 2021 - 11:15

Muhtasari


  • Akothee asema wasichana wenye ujauzito wanapaswa kuendelea na masomo
  • Hili linaashiria kwamba masomo ya wasichana wengi hukatizwa kwa ajili ya sababu kama hiyo
  • Lakini wanachosahau wengi ni kuwa ujauzito sio ugonjwa wala virusi

Mwanabiashara na msanii Esther Akoth maarufu Akothee amechangia katika mjadala unaoendelea nini kitakachofanyiwa wasichana ambao wanapata ujauzito bado wakiwa shule au wanaoendelea na masomo yao.

Kulingana na mwanamuziki huyo , wasichana wanaoenda shule wanaopata ujauzito hawapaswi kurudishwa nyumbani, na badala yake wanapaswa kuruhusiwa kuendelea na masomo isipokuwa afya yao itathibitisha vinginevyo.

Asilimia kubwa ya wasichana kuacha shule kwa ajili ya ujauzito imeshuhudiwa nchini hasa wakati wa janga la corona wasichana wengi hawakurudi shule zilipofunguliwa kwani walikuwa wajawazito.

Hili linaashiria kwamba masomo ya wasichana wengi hukatizwa kwa ajili ya sababu kama hiyo.

Lakini wanachosahau wengi ni kuwa ujauzito sio ugonjwa wala virusi.

"Na nadhani wasichana wote wanaopata mimba wakiwa shulenihawapaswi kupelekwa nyumbani

Lakini wanapaswa kuruhusiwa kuendelea na elimu isipokuwa afya yao itathibitisha vinginevyo. Mimba sio kufariki, ni usumbufu wa muda unaokuja na baraka kubwa. Unafikiria nini,"Alissema Akothee.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved