logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Akothee ambubujikia sifa baby daddy Mfaransa kwa kulea wanawe baada ya kuwalaki nchini

Mwanamuziki huyo alisema kuwa anawaheshimu sana 'baby daddies' wake ila anamheshimu zaidi babake Oyoo  kwani anafanya kusaidiana katika ulezi kuwa rahisi.

image
na Radio Jambo

Habari22 July 2021 - 07:55

Muhtasari


•Wawili hao walitua katika uwanja wa ndege wa JKIA usiku wakiandamana na baba mzazi wa Oyoo ajulikanaye kama Dominic ambaye wanaishi naye.

•Akitangaza kuwasili kwao kwenye mtandao wa Instagram, mama huyo wa watoto watano alimshukuru sana baba wa kitinda mimba  wake kwa kukubali ombi lake kuja Kenya kuwaona wazazi wake.

Papa Oyoo na Akothee

Akothee almaarufu kama Madam Boss ni mama mwenye furaha baada ya kuwapokea wanawe wawili Prince Ojwang na Prince Oyoo nchini kutoka Ufaransa.

Wawili hao walitua katika uwanja wa ndege wa JKIA usiku wakiandamana na baba mzazi wa Oyoo ajulikanaye kama Dominic na ambaye wanaishi naye.

Akothee ambaye alikuwa ameandamana na binti wake wawili Rue Baby na Vesha Okello kuwalaki alionekana mwenye bashasha si haba kuwaona wanawe baada ya kipindi kirefu.

Akitangaza kuwasili kwao kupitia mtandao wa Instagram, mama huyo wa watoto watano alimshukuru sana baba wa kitinda mimba  wake kwa kukubali ombi lake kuja Kenya kuwaona wazazi wake.

Akothee alisema kuwa atampeleka kijijini kwao Rongo ili wazazi wake wakamshukuru kwa kukubali kumsaidia kulea watoto.

"Shukran kwa kuheshimu ombi langu kuja kuonababangu kwani amekuwa akikuulizia. Kesho nakupela kwetu Rongo, kule nilikozaliwa wazazi wangu wakushukuru kwa kuwalea watoto wetu" Akothee alisema.

Mwanamuziki huyo alisema kuwa anawaheshimu sana 'baby daddies' wake ila anamheshimu zaidi babake Oyoo  kwani anafanya kusaidiana katika ulezi kuwa rahisi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved