logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Mimi ni mzima!" Familia ya Charles Njonjo yapuuzilia mbali uvumi kuwa amefariki

Ujumbe ambao ulitolewa na familia yake kwa vyombo vya habari umethibitisha kwa Njonjo ako salama salimini na anafurahia wikendi akiwa nyumbani kwake.

image
na Radio Jambo

Habari10 October 2021 - 06:16

Muhtasari


•Ujumbe ambao ulitolewa na familia yake kwa vyombo vya habari umethibitisha kwa Njonjo ako salama salimini na anafurahia wikendi akiwa nyumbani kwake.

•Uvumi kuhusu kifo cha mkongwe huyo wa miaka 101 ulienezwa sana mitandaoni siku ya Jumamosi

Mwanasiasa mkongwe Charles Mugane yu hai na buheri wa afya tofauti na madai yaliyoenezwa hapo awali kwamba ameaga dunia.

Familia ya mwanasheria huyo mkuu wa kwanza nchini imepuuzilia mbali uvumi kuhusu kufariki kwake na kudai kuwa ni ripoti zilizotiwa chumvi.

Ujumbe ambao ulitolewa na familia yake kwa vyombo vya habari siku ya Jumapili umethibitisha kwa Njonjo ako salama salimini na anafurahia wikendi akiwa nyumbani kwake.

"Ripoti kuhusu kifo changu zimetiwa chumvi. Niko buheri wa afya na nafurahia wikendi yangu nyumbani tunaposherehekea siku ya Utamaduni" Ujumbe huo ulisoma.

Uvumi kuhusu kifo cha mkongwe huyo wa miaka 101 ulienezwa sana mitandaoni siku ya Jumamosi.

Wengi walijipata wakiamini madai hayo kutokana na kiwango kiubwa cha ripoti kuhusu kifo chake ambazo zilichapishwa kwenye mitandao ya kijamii.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved